Baada ya Singapore kuunda gari la kwanza, hayati rais mstaafu Mzee Daniel Arap Moi alishawishika na kuitaka Kenya kufuata mkondo huo. Aliagiza Chuo Kikuu Cha Nairobi kuunda gari litakaloiweka Kenya kwenye ramani kama taifa linalotengeneza magari. Mradi wa nyayo kama ulivyotambulika hata hivyo haukufanikiwa huku wengi wakikosa kuelewa kilichosababisha kutofaulu kwake. Ben Kirui anaangazia mradi wa kuunda gari la kwanza nchini almaarufu nyayo pioneer.