المدة الزمنية 7:6

UDUMAVU NA UTAPIAMLO NI FEDHEHA- MEYA IRINGA

بواسطة Makutano TV
124 مشاهدة
0
3
تم نشره في 2021/05/24

Ni katika kikao Cha utekelezaji wa viashiria vya mkataba wa Lishe katika kata 18 zilizopo Manispaa ya Iringa. Katika kikao hiki zipo changamoto kadhaa zilizobainishwa na Afisa Lishe Manispaa ya Iringa Bi Anzael Msigwa ikiwemo ucheleweshwaji katika kuibua watoto wenye utapiamlo kwenye mitaa. Changamoto nyingine ni kukosekana kwa taarifa katika mbao za matangazo ofisi za kata. Meya wa Manispaa ya Iringa Ibrahimu Ngwada amekemea tabiaa ya baadhi ya wazazi kutowajjibika katika suala la malezi huku akisisitiza kuwa suala la udumavu na utapiamlo ni fedheha. Mkakati wa utekelezaji wa viashiria vya Lishe ngazi ya kata na mitaa unahusisha kata ya Nduli, Kihesa, Mtwivila, Mkimbizi, Gangilonga, Mkwawa, Ilala, Makorongoni, Mivinjeni, Isakalilo, Mlandege, Mwangata, Kwakilosa, Kitwiru, Igumbilo, Ruaha, Kitanzini na Mshindo

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 0